Friday 2 January 2015

Leave a Comment

JINSI YA KUDUMISHA UHUSIANO WA MBALI.

JINSI YA KUDUMISHA UHUSIANO WA MBALI.

Siku zote mapenzi huyapa maisha thamani lakini wapo ambao hujikuta kwa namna moja ama
nyingine wanatengana na wapenzi wao kwa sababu tu ya mihangaiko ya kila siku ya kujitafutia ridhiki.
Masomo na wakati mwingine utengano huwa ni matokeo ya wapendanao kuishi sehumu tofauti hii huwakumba sana
wanafunzi wa vyuo na skuli za bweni(hostel).

Umbali hulifanya penzi baina ya wapendanao kuteteleka kama wapendanao hawatafanya kazi
za ziada kuhakikisha wanaziba mianya yote itakayosababisha usaliti kama sio kuachana kabisa.

Hata hivyo, mapenzi ya mbali huna ni vigumu kuteteleka endapo tu wapendanao wanamapenzi ya dhati na kutamani kuwa pamoja
kila wakati na mmoja wapo kuamua kujitoa muhanga kwa kuamia anakoishi ama kufanyia
kazi la azizi wake.

Hata hivyo, mnaweza kudumisha mapenzi yenu ya mbali endapo
utafanya haya:-

MAWASILIANO MARA KWA MARA.

Mawasiliano ni nguzo muhimu sana baina ya wapendanao, humfanya kila mtu kuhisi uwepo
wa mwenzi wake hata kama atakuwa mbali naye.

Hivyo, kama una mpenzi wako aliye mbali nawe hakikisha unakuwa naye karibu kwa kumtumia ama sms, email, kadi au simu.

Aidha, pindi mnapowasiliana hakikisha humkwazi mwenzako kwa namna yoyote ile,kwani kuna watu wengi wanatabia ya kudharau baadhi ya mambo kutokana na kutingwa na
shughuli kadha wa kadha, naomba nikuweke wazi kuwa hata kama umebanwa vipi pindi mpenzi wako aliyembali anapokutumia ujumbe kwenye simu yako basi usisite kumjibu katika muda muafaka na siyo kuuchuna hadi
ulalamikiwe!

HESHIMU HISIA ZAKO:

Mapenzi ya kweli yametawaliwa na hisia kali ambazo ndizo huwafanya wapendanao kufikishana kwenye mambo fulani kwani pasipo hisia hata uwe na ujuzi au utundu wakutosha
hutapata raha ya mapenzi.

Kama kweli unampenda kwa dhati mwenza wako na mmetengana kutokana na sababu za kimasomo ama kazi kwa hakika utakuwa tayari kumtunzia penzi lake hadi mtakapokutana tena.

Uaminifu pekee ndio utakaokufanya uwasiliane mara kwa mara na mwenza wako na kwenye uaminifu mapenzi hushamiri huku kila mmoja akimuonea wivu wa hapa na pale mwenzi wake.

Lakini sio ule wakubomoa! Hivyo heshimu hisia zako kama kweli unampenda mwenzi wako kwa
kumuonyeshe unampenda.

UMBALI ISIWE KIGEZO KUNYIMANA.

Mpe mwandani wako raha kamili kama ilivyokuwa awali mlipokuwa pamoja!
Bila shaka unajiuliza inawezekanaje? Hili linawezekana kwa kutumia njia yoyote ya mawasiliano.
Mfano kama nyote mna simu jiandaye vyakutosha nikiwa na
maana uhakikishe upo sehemu ambayo utakuwa huru kuongea ama kufanya chochote
Kitakachokufanya uhisi raha isiyo na kifani na kukufikisha kwenye kilele cha mlima kilimanjaro
bila kutarajia.

Bila shaka kila mtu anamfahamu vema mpenzi wake na hasa nini hupenda kufanyiwa ili aweze
kufika safari yake na kama ndivyo basi hakikisha unafanya mambo yote ambayo ukimfanyia
mwenzi wako pindi mnapokuwa kwenye mambo fulani hupagawa.

Nawasilisha hoja!
Siku zote mapenzi huyapa maisha thamani lakini wapo ambao hujikuta kwa namna moja ama
nyingine wanatengana na wapenzi wao kwa sababu tu ya mihangaiko ya kila siku ya kujitafutia ridhiki.
Masomo na wakati mwingine utengano huwa ni matokeo ya wapendanao kuishi sehumu tofauti hii huwakumba sana
wanafunzi wa vyuo na skuli za bweni(hostel).

Umbali hulifanya penzi baina ya wapendanao kuteteleka kama wapendanao hawatafanya kazi
za ziada kuhakikisha wanaziba mianya yote itakayosababisha usaliti kama sio kuachana kabisa.
Hata hivyo, mapenzi ya mbali huna ni vigumu kuteteleka endapo tu wapendanao wanamapenzi ya dhati na kutamani kuwa pamoja
kila wakati na mmoja wapo kuamua kujitoa muhanga kwa kuamia anakoishi ama kufanyia
kazi la azizi wake.
Hata hivyo, mnaweza kudumisha mapenzi yenu ya mbali endapo
utafanya haya:-
MAWASILIANO MARA KWA MARA.
Mawasiliano ni nguzo muhimu sana baina ya wapendanao, humfanya kila mtu kuhisi uwepo
wa mwenzi wake hata kama atakuwa mbali naye.
Hivyo, kama una mpenzi wako aliye mbali nawe hakikisha unakuwa naye karibu kwa kumtumia ama sms, email, kadi au simu.
Aidha, pindi mnapowasiliana hakikisha humkwazi mwenzako kwa namna yoyote ile,kwani kuna watu wengi wanatabia ya kudharau baadhi ya mambo kutokana na kutingwa na
shughuli kadha wa kadha, naomba nikuweke wazi kuwa hata kama umebanwa vipi pindi mpenzi wako aliyembali anapokutumia ujumbe kwenye simu yako basi usisite kumjibu katika muda muafaka na siyo kuuchuna hadi
ulalamikiwe!
HESHIMU HISIA ZAKO:
Mapenzi ya kweli yametawaliwa na hisia kali ambazo ndizo huwafanya wapendanao kufikishana kwenye mambo fulani kwani pasipo hisia hata uwe na ujuzi au utundu wakutosha
hutapata raha ya mapenzi.
Kama kweli unampenda kwa dhati mwenza wako na mmetengana kutokana na sababu za kimasomo ama kazi kwa hakika utakuwa tayari kumtunzia penzi lake hadi mtakapokutana tena.
Uaminifu pekee ndio utakaokufanya uwasiliane mara kwa mara na mwenza wako na kwenye uaminifu mapenzi hushamiri huku kila mmoja akimuonea wivu wa hapa na pale mwenzi wake.
Lakini sio ule wakubomoa! Hivyo heshimu hisia zako kama kweli unampenda mwenzi wako kwa
kumuonyeshe unampenda.
UMBALI ISIWE KIGEZO KUNYIMANA.
Mpe mwandani wako raha kamili kama ilivyokuwa awali mlipokuwa pamoja!
Bila shaka unajiuliza inawezekanaje? Hili linawezekana kwa kutumia njia yoyote ya mawasiliano.
Mfano kama nyote mna simu jiandaye vyakutosha nikiwa na
maana uhakikishe upo sehemu ambayo utakuwa huru kuongea ama kufanya chochote
Kitakachokufanya uhisi raha isiyo na kifani na kukufikisha kwenye kilele cha mlima kilimanjaro
bila kutarajia.
Bila shaka kila mtu anamfahamu vema mpenzi wake na hasa nini hupenda kufanyiwa ili aweze
kufika safari yake na kama ndivyo basi hakikisha unafanya mambo yote ambayo ukimfanyia
mwenzi wako pindi mnapokuwa kwenye mambo fulani hupagawa.
Nawasilisha hoja!

0 comments:

Post a Comment