Friday 2 January 2015

Leave a Comment

VITU VINAVYOSHANGAZA KUHUSU WANAWAKE.


.
.
*Unaweza dhani kwakuwa wanaujua uchungu,shida na mateso ya mimba na adha ya kumbeba mtoto,wangekuwa wa kwanza kumpisha seat mwanamke mwenzao mjamzito au aliembeba mtoto.Lakini ni kinyume kabisa na h...ivyo.Wanaume ndio wa kwanza kuwapa seat wanawake wa aina hiyo.
*Pili. Unaweza dhani kwa kuwa wamepitia leba kwenye uchungu mkali ili kupata watoto watakuwa wakarimu na wenye upendo kwa mtoto yeyote duniani.Lakini ni kinyume kabisa na hivyo.Takwimu zinaonyesha kuwa ukatili unaofanywa kwa watoto,kama kuchomwa miili yao,kukatwa vidole na vingine kama hivyo,hufanywa na wanawake zaidi kuliko hata wanaume ambao hawajui hata leba zipo upande gani wa Hospitali.
*Tatu. Unaweza dhani kwa kuwa wao kama wanawake wanajua vizuri shida zinazowakabili kuliko kundi lingine kuanzia ndani kifamilia mpaka nje kijamii,basi watamsapot mwanamke mwenzao aingie madarakani ili awawakilishe.Lakini ni kinyume kabisa na hivyo.Wao ndio chombo cha kwanza kinachotumiwa na wanaume kuwaharibu wanawake wenzao wanaoonyesha nia na uthubutu wa kushika madaraka na kuwakomboa.
Nne. Unaweza dhani kwamba changamoto nyingi zinazowakabili katika mazingira hatarishi zitawajenga na kuwafanya wawe watulivu na wenye ufanisi katika kufanya maamuzi.Lakini ni kinyume kabisa na hivyo.Wengi wao hukurupuka kwenye kufanya maamuzi.Hawajiamini na hukikososa hata kile wanachohisi ni sahihi.Na ni kawaida kwao kuendeshwa na mawazo ya watu wengine,hasahasa mashoga zao.Huku kibaiolojia tukiambiwa mwanamke ana wigo mpana wa kufikiri kuliko mwanaume.
Tano. Unaweza dhani kwamba uzuri wao wa nje unahakisi kitu kikubwa na cha kuvutia kichwani,kiasi kwamba kikamvutia mtu kuwa naye karibu na kuvuna mawazo ya maana toka kwake.Lakini ni kinyume kabisa na hivyo.Wanapoteza muda wao mwingi kuutafuta uzuri tena kwa gharama yeyote kuliko kutafuta maarifa kwa ajili ya maisha yao.Mwishowe huishia kuutumia huo uzuri kwa njia isiyo stahili kwa kuwa sehemu ya maarifa imekaliwa na urembo usio na maana.

0 comments:

Post a Comment